Mheshimiwa Kairuki akizungumza na msafara wa wafanyabiashara kutoka Ujerumani kampuni ya Bosch na wawakilishi wa taasisi za Serikali kwenye ukumbi wa mikutano wa TIC. |
Akizungumza katika mkutano huo, Mhe.
Kairuki ameishukuru kampuni ya Bosch kwa kufikiria kuwekeza Tanzania na kwamba
uamuzi wao sio wa bahati mbaya bali ni hakika kutokana na mazingira mazuri ya
uwekezaji yaliyopo, soko la uhakika na utayari wa serikali katika kuwasaidia
kufanikisha miradi wanayotarajia kuianzisha ikiwamo kupata vibali na leseni za
uwekezaji zinazotolewa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) chini ya mfumo wa
Huduma za Mahala Pamoja ‘One Stop Facilitation Centre’. Vilevile Mhe.
Waziri ameainisha fursa na maeneo ya uwekezaji kwa kampuni hiyo kuwa ni
viwanda, madini, tehama, kuunganisha magari, kuzalisha na kusambaza umeme,
mafuta na gesi.
Mhe.
Waziri akijadiliana jambo na Naibu Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Jörg
Herrera (katikati) pamoja na Bw.Uwe Uwe
Raschke
|
Katika kuhakikisha kwamba ujumbe huo
unapata taarifa na ufafanuzi zaidi kuhusu fursa zilizopo na miradi/maeneo
ambayo nchi inaweza kushirikiana na kampuni ya Bosch, taasisi mbalimbali za
serikali zilishiriki ili kuelezea. Taasisi zilizoshiriki ni Wizara ya Madini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, Shirika la Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
(TAA), Shirika la Reli Tanzania (TRC), Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), Wakala
wa Ujenzi (TBA) na wenyeji Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC). Aidha Mhe.
Kairuki pia amewataka sekta binafsi kuchangamkia fursa hii na kuangalia namna
ambavyo wanaweza kushirikiana na kampuni ya Bosch katika biashara na uwekezaji
kwenye maeneo yaliyoainishwa.
Tayari baadhi ya vifaa vya kampuni ya Bosch
vimenunuliwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania kwa lengo la kutumika
kwenye uendeshaji wa shughuli mbalimbali katika uwanja mpya Terminal 3,
Julius Nyerere Airport.
Wawakilishi wa taasisi za serikali walishiriki kikao cha Mhe Kairuki na ugeni kutoka Ujerumani |
Kampuni ya Bosch
imekuwepo Afrika katika nchi takribani 13 lakini bado ilikuwa haijafanya
uwekezaji Tanzania. Hivi sasa kampuni hii imeridhishwa na kuvutiwa na mazingira
ya uwekezaji yaliyopo nchini na yamewashawishi kufanya maamuzi ya kuja
kuwekeza. Taasisi za serikali na sekta binafsi zijipange kutoa ushirikiano
utakaohitajika kwa kwa kampuni hii ili kufanikisha uwekezaji wao unaotarajiwa
kuleta uwekezaji wa ubia, tekinolojia, uzalishaji wa bidhaa bora zenye gharama
nafuu, kutengeneza ajira na kuongeza pato la Taifa kiujumla.
Timu ya ujumbe wa wafanyabiashara kutoka Ujerumani katika kikao cha pamoja na Mhe Waziri Kairuki |
0 Comments