Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Utafiti wa Kahawa ni muhimu ktk Uwekezaji


Sekta ya kilimo ni muhimu kwa uchumi wa Taifa letu, na ni muhimu kwa Mtanzania mmoja mmoja kutokana na kuwa ni nguzo ya uhai wa viumbe kutokana na uzalishaji wa chakula ambacho kila mmoja wetu hukitumia..yaani uwe Tajiri au Masikini utaitegemea tu sekta hii kwani uhai wako ndipo ulipo.



Anaandika Grace Semfuko.



Asilimia kubwa ya Watanzania waishio vijijini hutegemea sekta hii kama shughuli kuu ya kiuchumi na ndio maana shughuli nyingi za kilimo hufanywa huko Vijijini, inakadiriwa kuwa zaidi ya robo tatu ya Watanzania wanajishughulisha na kilimo cha mazao mbalimbali yakiwepo ya chakula pamoja nay ale ya kibiashara.



Kahawa ni mojawapo ya mazao makuu ya biashara nchini Tanzania.



Kahawa ni zao muhimu la kibiashara ambalo hulimwa katika Mikoa ya Kaskazini na Nyanda za Juu Kusini. Mikoa inayolima Kahawa ni pamoja na Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Tanga, Morogoro, Mbeya, Songwe, Iringa na Ruvuma katika Wilaya ya Mbinga, Kigoma, Tarime na Bukoba.



Zao la Kahawa hulimwa kama zao la kibiashara mbali na kuwapatia watu kipato kikubwa ambacho huwasaidia katika kutatua changamoto mbalimbali za kiuchumi pia husaidia katika kupambana na umasikini.



Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) imekuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya Kahawa kuwa yenye manufaa na endelevu, TaCRI  imetafiti na kuainisha teknolojia muafaka za kilimo cha kahawa ambapo tayari imeshatoa aina 19 za kahawa aina ya Arabika na Robusta ambazo hazishambuliwi na magonjwa ya Chulebuni (CBD) na kutu ya majani ambazo zimesaidia kuongeza tija kwa mti.



Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) Dkt Deusdedit Kilambo anasema taasisi hiyo imekuwa ikitoa mafunzo katika ngazi ya vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) yanayohusu kilimo bora cha zao hilo ili kuinua zaidi kilimo bora cha zao hilo ili kuinua zaidi kilimo cha kahawa.



Kwa mujibu wa Dkt Kilambo Taasisi yake imejipanga kukidhi mahitaji ya miche ya kahawa kitaifa kwa kushiriki katika uzalishaji wa miche milioni sita kwa mwaka kwa kushirikiana na vyama vya msingi pamoja na wadau wengine.



Dkt Kilambo anasema TaCRI imejipanga kuzalisha miche zaidi, kutoa mafunzo kwa Wakulima na maafisa ugani ili kuendesha kilimo cha Kahawa kibiashara.



Anabainisha kuwa uwepo wa maabara ya kisasa katika kituo chao ambayo hupima hali ya udongo imekuwa na msaada mkubwa kwao kutokana na kufanya uchanganuzi wa udongo wa mimea na kutoa ushauri unaofaa katika kuongeza tija ya zao la kahawa kwa wakulima.



Kwa upande wake Mtafiti wa usambazaji wa teknolojia na mafunzo TaCRI Bi Sofia Malinga anasema mafunzo hayo yanahusisha kufanya utafiti wa kuendeleza zao la kahawa kupitia mipango mbalimbali ambapo tayari taasisi hiyo imetoa aina 19 bora za kahawa aina ya Arabika na 4 aina ya Robustaambazo hazishambuliwi na magonjwa ya chulebuni (CBD) na kutu ya majani.



“TaCRI imetoa aina hizo mpya za kahawa ambazo ni mafanikio ya kipekee kwani zimekuwa ni mkombozi mkubwa kwa mkulima na chimbuko kubwa la mapinduzi ya kijani kwani uwepo wa mbegu hizo mpya umechangia katika kuongeza ubora wa kahawa ikiwa ni pamoja na kumuonngezea mkulima kipato” anasema Maliga.



Anafafanua kuwa TaCRI imetafiti na kupendekeza teknolojia muafaka za kuzalisha miche aina bota ya chotara ambapo wanazalisha miche kwa njia ya chupa.



Akizungumza katika ufunguzi wa maonesho ya 26 ya nanenane Kanda ya Kaskazini, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Anna Mgwira anawataka maofisa ugani wa mikoa ya Kanda hiyo kuacha utamaduni wa kuandaa maonesho kama nia ya kuwaridhisha viongozi na Wananchi wanaotembelea maonesho hayo na badala yake waendane na uhalisia wa bidhaa zinazozalishwa na Wakulima Vijijini.



Nae Mrajis wa Msaidizi wa vyama vya Ushirika Mkoa wa Kilimanjaro John Henjewele anasema moja kati ya msisitizo wa Serikali ya awamu ya tano ni kuwataka Wakulima kuzalisha mazao yenye tija ya kiuchumi ili kuondokana na umasikini.



“Mkakati wa Serikali ni kuhakikisha mazao matano ya kimkakati ambayo ni Kahawa, Korosho, Tumbaku, Pamba na Chai uzalishaji wake unaongezeka” alisema Henjewele alipotembelea banda la TaCRI kwenye maonyesho ya Kilimo.


Post a Comment

0 Comments