Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Tanzania ni salama-Rais Magufuli

Ripoti ya Global Peace Index ya mwaka 2020 imeitaja Tanzania kushika nafasi ya kwanza kwa Amani na Utulivu kwenye nchi za Afrika Mashariki na nafasi ya sabakwa nchi zilizopo kusini mwa Jangwa la Sahara, kwa niaba ya Watanzania wote navipongeza vyombo vya ulinzi na usalama Rais Magufuli wakati akihutubia Bunge.

Mojawapo ya ahadi kubwa niliyoitoa wakati nazindua Bunge ilikuwa Amani na utulivu wa nchi yetu, ninayo furaha kulitaarifu bunge lako kwamba nimeitimiza ahadi hiyo kwa vitendo, Muungano wetu umeendelea kuimarika, tumeweza kushughulikia changamoto za muungano ikiwepo kufuta kodi mbalimbali.

Tumefanikiwa kulinda mapinduzi matukufu ya Zanzibar, nchi yetu imeendelea kuwa kisiwa cha Amani na mipaka yake imeendelea kuwa salama, tulipoingia madarakani kulikuwepo na wimbi la ujambazi na mauaji ya kibiti, kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na jeshi la ulizni na usalama, vitendo hivyo vilikomeshwa na sasa Tanzania iko salama.
TUENDELEE KUWEKEZA TANZANIA, HII NI KIELELEZO TOSHA KUWA WAWEKEZAJI KUWA SALAMA

Post a Comment

0 Comments