Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Tanzania yavutia wawekezaji kutoka Saudi Arabia





Baadhi ya wawekezaji kutoka Saudi Arabia wakifuatilia  mkutano


  Ujumbe wa wafanyabiashara na maafisa wa Serikali wapatao 15 kutoka Saudi Arabia wamewasili nchini kwa lengo la kuangalia fursa za biashara na uwekezaji. Wafanyabiashara waliowasili wanawakilisha makampuni yapatayo saba kwenye sekata za ujenzi, nishati, viwanda, makazi, madawa na tehama. Wafanyabiashara hao watakuwa nchini kwa muda wa siku mbili ili kupata taarifa za awali za biashara na uwekezaji zitakazowashawishi kuwekeza nchini.

Majina ya makampuni kutoka Saudi Arabia
   

   Ili kuhakikisha kwamba wafanyabiashara hao wanapata taarifa za awali juu ya fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini sambamba na namna ambavyo  watasaidiwa kuanzisha miradi yao hapa nchini Taasisi ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA)  kwa kushirikisha Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Ubalozi wa Saudi Arabia nchini wameandaa mkutano wa biashara ‘business meeting’ tarehe 30 Januari, 2019 New Afrika Hotel. Siku ya pili wafanya biashara hao wataendelea na mikitano ya ana kwa ana pamoja na kutembelea baadhi ya viwanda.

Afisa Uhamasishaji Uwekezaji wa TIC Bi. Diana Ladislaus akitoa mada ya mazingira na fursa za uwekezaji 




   Mkutano huo uliandaliwa katika sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza asubuhi ilihusisha wafanyabiashara hao pamoja na taasisi za serikali na sekta binafsi za Tanzania kwa lengo la kutoa mawasilisho na kuendesha mijadala mbalimbali fursa za biashara na uwekezaji pamoja na taratibu za kuanzisha miradi nchini.  Taasisi za Serikali na sekta binafsi zilizoshiriki ni pamoja na TIC, BRELA, SIDO na TCCIA. Kituo cha Uwekezaji Tanzania kilipata nafasi ya kutoa mada juu ya fursa na mazingira ya uwekezaji nchini na mada iliwasilishwa na Bi. Diana Ladislaus, Afisa Uhamasishaji Uwekezaji.

Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji wa TIC Bw. John Mnali akizungumza na vyombo vya habari wakati wa mkutano wa kibiashara na wawekezaji kutoka Saudi Arabia.


  

   Sehemu ya pili ya mkutano huo ilifanyika mchana ikihusisha mikutano ya ana kwa ana ‘B2B meetings’ kati ya wawakilishi wa makampuni ya Kitanzania na Saudi Arabia kwa lengo la kujadili fursa za uwekezaji, biashara na uanzishaji wa miradi ya pamoja/ubia.
Sehemu ya wafanyabiashara wa Kitanzania wakijadilianana wafanyabiashara wa Saudi Arabia kuhusu fursa za biashara na uwekezaji
   Kituo cha Uwekezaji Tanzania kimefurahishwa na ujio wa wafanyabiashara hao kwa matarajio kwamba endapo  watafikia maamuzi ya kuanzisha miradi yao, nchi itanufaika kwa kuongeza pato la Taifa kupitia ajira zitakazozalishwa, kodi itakayokusanywa, uzalishaji wa bidhaa nchini na kuvutia tekinolojia mpya.




Post a Comment

0 Comments