Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

‘TIC yaikaribisha nchini kampuni ya TDH ya Uholanzi iliyobobea katika biashara na uwekezaji kwenye zao la korosho’.




Katika jitihada za kutafuta/kuhamasisha na kuvutia wawekezaji nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Geoffrey Mwambe yupo nchini Uholanzi ambapo amepokelewa na Mwenyeji wake Mhe. Irene Kasyanju Balozi wa Tanznaia Uholanzi kwa lengo la kufanya ziara ya kikazi itakayochukua takribani siku tano kuanzia tarehe 4 Februari, 2019. Akiwa na Mhe. Balozi, Mwambe atakutana na uongozi wa makampuni makubwa yenye nia ya kuwekeza Tanzania na kufanya nao mazungumzo ya kimkakati yenye lengo la kuwavutia kuja kuwekeza Tanzania kwenye sekta za kipaumbele.

Bw. Geoffrey I. Mwambe Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Mheshimiwa Irene Kasyanju, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uholanzi, Bw. George Mukono Afisa Uwekezaji Mwandamizi kutoka TIC wakiwa katika mazungumzo na uongozi wa kampuni ya Trade and Development Holding B.V. (TDH) ambayo imeonesha nia ya kujenga kiwanda cha korosho nchini Tanzania.  

Katika hatua za awali, Mkurugenzi Mtendaji pamoja na Mhe. Balozi wamefanya mazungumzo na Bw. Kees Blokland Mkurugenzi wa Biashara aliyeambatana na maafisa wengine wawili kutoka kampuni ya Trade and Development Holding B.V. (TDH). TDH ni kampuni kubwa na maarufu nchini Uholanzi inayojihusisha na biashara ya korosho duniani. Kampuni hii imewahi kufanya biashara ya korosho nchini Tanzania na sasa imefanya uwekezaji kwenye viwanda vya korosho nchini Burkina Faso na Benin. 

Pichani ni timu ya Tanzania ilipokutana na uwakilishi wa kampuni ya TDH nchini Uholanzi. Kutoka kushoto ni; Bw. Kees Blokland Mkurgenzi na Bw. Ronald Zaal Meneja uendeshaji wa Trade and Development Holding B.V. (TDH). Kati ni Geoffrey I. Mwambe Mkurugenzi Mtendaji wa TIC akifuatiwa na Mheshimiwa Irene Kasyanju, Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi na mwisho Bi. Agnes K. Tengia, Afisa Ubalozi nchini Uholanzi.  
Kwa kuzingatia hayo, Mkurugenzi Mtendaji amefanya mazungumzo na uongozi wa kampuni hiyo ili kuwakaribisha kwa mara nyingine kufikiria kuja Tanzania kwa ajili ya kuwekeza katika zao la korosho. Mkurugenzi wa TDH amesema anatambua ubora wa korosho kutoka Tanzania na mazingira ya uwekezaji yaliyopo kwa sasa. Kwa niaba ya kampuni hiyo ameonesha utayari wa kurejea nchini kwa ajili ya kuwekeza katika zao la korosha hususan kujenga kiwanda cha kubangua korosho. Katika hatua za awali, kampuni hii itawasilisha andiko mradi (Business Proposal) likielezea nia ya kujenga kiwanda cha korosho nchini. Hata hivyo jambo litafanyika baada ya kampuni ya TDH kukamilisha majadiliano na Taasisi za kifedha nchini Uholanzi ‘The Netherlands Development Finance Company’ (FMO). 

Ujio wa kampuni hiyo utakuwa wa manufaa kwa Taifa kwani utaleta mabadiliko chanya katika zao la korosho kwa kuwa kiungo cha kuongeza chachu kwenye mnyororo wa thamani wa zao hilo la biashara. 
Bw. Kees Blokland Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Trade and Development Holding B.V. (TDH) (kulia)akifurahia zawadi ya majani ya chai kutoka Tanzania aliyokabidhia na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC ikiwa ni sehemu ya kuitangaza bidhaa zinazozalishwa nchini Tanzania.



Post a Comment

0 Comments