Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI ANGELLAH KAIRUKI AKARIBISHA RAIA WA MISRI KUWEKEZA TANZANIA


Na Latiffah Kigoda TIC, Dar Es Salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki amesema ipo haja kwa wawekezaji kutoka Nchini Misri kuwekeza Tanzania kwa kuwa kuna mazingira mazuri ya uwekezaji pamoja na fursa mbalimbali kwenye sekta uwekezaji.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akifanya mazungumzo na Balozi wa Misri Nchini Tanzania Bw.Mohammed Abulwafa, wengine ni Maafisa kutoka Wizarani pamoja na Maafisa kutoka katika Ubalozi huo

Kairuki amesema Ofisi yake na Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC wanafanya kazi kubwa ya kuhakikisha wawekezaji wanapata nafasi ya kuwekeza katika sekta zote ikiwepo ya Viwanda, Kilimo, Ujenzi, Mifugo, Dawa na Vifaa tiba na uongezaji wa thamani wa bidhaa mbalimbali.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akisalimiana na Balozi wa Misri Nchini Tanzania Bw.Mohammed Abulwafa.
Waziri Kairuki aliyasema hayo mapema leo alipofanya mazungumzo na Balozi wa Misri nchini Tanzania Bw. Mohammed Abulwafa ambaye alimtembelea ofisini kwake akiambatana na Msimamizi wa masuala ya biashara wa Ubalozi huo Bw.Mohemmed Meguid pamoja na Katibu wake Bw.Ahmed Ghoul.

Post a Comment

0 Comments