Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Waziri Kairuki akutana na Mabalozi Watatu wa nje kuzungumzia Uwekezaji






Na Latiffah Kigoda-TIC,Dar Es Salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Mhe. Angellah Kairuki leo 3 Oktoba,2019 ameonana na kufanya mazungumzo mafupi kwa nyakati tofauti na Mabalozi wa nchi tatu leo katika Ofisi Ndogo za Wizara zilizopo, Dar as Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akisalimiana na Balozi wa Denmark Nchini Tanzania Bi Mette Noergaard.
(Picha na Latiffah Kigoda-Afisa Habari TIC)

Mabalozi hao ni pamoja na Mhe. Shinichi Goto (Balozi wa Japan), Mhe. Mette Noergaard, (Balozi wa Denmark) na Mhe. Jeroen Verhoeven (Balozi wa Uholanzi) hapa nchini.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akisalimiana na Balozi wa Uholanzi Mhe.Jeroen Verhoeven.
(Picha na Latiffah Kigoda-Afisa Habari TIC)

Waziri Kairuki ametumia fursa ya kukutana na Mabalozi hao kuendelea kuwakaribisha Wawekezaji kutoka katika nchi wanazowakilisha Mabalozi hao hususani katika kipindi hiki ambacho Serikali ya Awamu ya Tano inafanya jitihada za dhati katika kuboresha mazingira ya Uwekezaji na kufanya biashara nchini.

 Kwa upande wao Mabalozi hao walitumia fursa ya kukutana na Waziri huyo wa Uwekezaji kueleza mikakati mbalimbali waliyojiwekea katika kuhakikisha Wawekezaji wakubwa kutoka nchi zao wanachangamkia fursa mbalimbali za Uwekezaji zilizopo Tanzania.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akisalimiana na Balozi wa Japan Nchini Tanzania Bw.ShinichiGoto.
(Picha na Latiffah Kigoda-Afisa Habari TIC)

 Balozi wa Denmark, Mhe. Mette kwa kipekee alipongeza jitihada zinazofanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) katika kusikiliza na kufanyia kazi maoni ya wadau mbalimbali kunakolenga kuweka mazingira bora zaidi ya Uwekezaji nchini Tanzania na kwamba wataendelea kuunga mkono jitihada hizo.




Post a Comment

0 Comments