Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI KAIRUKI ATETA NA RAIS WA TCCIA

Na Latiffah Kigoda,TIC Dar Es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Angellah J. Kairuki amekutana leo na ujumbe kutoka Chemba ya Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) ulioongozwa na Bw. Koyi Rais mpya wa Chemba hiyo.Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kililenga kujadili masuala mbalimbali hususan namna Chemba hiyo inavyoweza kuendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali katika kukuza maslahi ya Sekta Binafsi nchini.
 Katika kikao hicho Bw. Koyi alifafanua kwa Waziri Kairuki namna ambavyo TCCIA inavyoratibu maslahi ya sekta binafsi nchini ambapo kwa sasa ni moja ya vyama vinavyosimamia sekta binafsi vyenye mtandao mpana kote nchini. Aidha, aliongeza kuwa kupitia mtandao huo wameweza kuwaunganisha wafanyabiasahara na wawekezaji kuanzia ngazi ya Taifa, Mikoa hadi Wilaya. Vilevile, alibainisha kuwakama sehemu ya kupanua huduma za Chemba hiyo





 
                Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki                  akisikiliza jambo kutoka kwa Mwenyekiti wa TCCIA chemba ya Mtwara Bw.Swallah Swallah

TCCIA sasa wamefungua matawi nje ya nchi kama vile Uingereza, Uturuki, China na Urusihatuailiyopelekea kupanua wigo na kuwafikia kwa karibu zaidi wadau wake wa nje ya nchi na hivyo kuwarahisishia utaratibu wa kufanya biashara na kuwekeza nchini. 
 Aidha, Rais huyo wa TCCIA alimweleza Waziri Kairuki kuwa yeye baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa Chemba hiyo alihamasika kuomba kukutana naye kwa kutambua umuhimu wa kufanya kazi kwa karibu na Serikali, hususaniOfisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) katika kutetea maslahi ya sekta binafsi nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akisalimiana na Rais wa TCCIA Bw. Paul Koyi wakiwa katika picha ya pamoja ya viongozi wa TCCIA ofisini kwa Waziri.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kazi kubwa iliyofanya ya kuandaa mikutano ya  mashauriano kati ya Serikali na wafanyabiashara na wawekezaji katika mikoa ya Ruvuma, Mtwara na Lindi ambapo alitaarifu kuwa Chemba yake ilishiriki kikamilifu katika maandalizi yake na kuwakilishwa na viongozi wa ngazi za mikoa kwenye Mikutano. Aliongeza kuwa Mikutano hiyo imeamsha ari ya wafanyabiashara na wawekezaji kufanya shughuli zao kwa kujiamini huku wakitambua kuwa sasa Serikali imekuwa sikivu kwa kusikiliza  changamoto zao na kuzitatua.
 Vilevile aliahidi kuwa Chemba itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu kwa Serikali hususani katika kipindi hiki ambapo kuna mchakato wa kufanya mapitio ya sera na sheria mbalimbali zinazolenga kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji hapa nchini. 
 Kwa upande wake,Waziri Kairukialimshukuru Bw. Koyi na wajumbe alioambatana naokwa kutenga muda wao kuja kuonana naye na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu kukuza sekta binafsi nchini. Aliongeza Serikali inatambua umuhimu wa sekta binafsi kama injini ya uchumi na ni wajibu wake kuhakikisha inaweka mazingira wezeshi na rafiki ili kukuza wawekezaji waliopo na kuvutia wengine wapya wa nje na ndani ya nchini. Pia,aliwashauri kuwaasa wanachama wao kushiriki kimamilifu katika kutoa maoni yao katika michakato ya mapitio ya sera ya sheria stahiki ili nchi ipate sheria itakayokidhi mahitaji kwa wakati huu na wakati ujao.

Post a Comment

0 Comments