Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Dkt Abbasi; Serikali imeimarisha mazingira ya uwekezaji

Na Grace Semfuko
Dar Es Salaam.
Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt Hassan Abbasi amesema Serikali imeimarisha mazingira ya uwekezaji kwa kuondoa urasimu, rushwa na baadhi ya tozo ili kuwarahisishia wawekezaji kufanya shughuli zao kwa urahisi Zaidi.
Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt Hassan Abbasi akizungumza na Waandishi wa Habari mapema leo Novembe 6,2019 kuhusu mafanikio ya miaka minne ya Rais Magufuli akiwa madarakani, Rais alichaguliwa na Watanzania kuongoza nchi Oktoka 25 mwaka 2015 na kuapishwa Novemba 5 mwaka huo huo wa 2015.(Picha na Grace Semfuko)
Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt Hassan Abbasi akizungumza na Waandishi wa Habari mapema leo Novembe 6,2019 kuhusu mafanikio ya miaka minne ya Rais Magufuli akiwa madarakani. (Picha na Grace Semfuko)
Amesema Serikali imeimarisha mifumo ya Sheria na Sera za uwekezaji ambapo sasa mwekezaji atanufaika Zaidi kutokana na kuondoa kabisa mianya ya rushwa iliyokuwa ikiwasumbua na kusababisha wakati mwingine uwekezaji kukwama.

Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt Hassan Abbasi akizungumza na Waandishi wa Habari mapema leo Novembe 6,2019 kuhusu mafanikio ya miaka minne ya Rais Magufuli akiwa madarakani. (Picha na Grace Semfuko)
“Tumejitahidi sana kuweka vivutio, nchi yetu ina Amani na utulivu, na ukiwauliza wawekezaji wengi kama kuna maeneo yalikuwa yanawakwaza ni urasimu na rushwa,na upatikanaji wa vitu kama ardhi, umeme na dawa, sasa hivi hayo hayapo tena” alisema Dkt Abbasi
“Nchi hii kila mwekezaji makini anajua, pale TIC tumeweka huduma zote kwenye ofisi moja, hakuna habari ya kutoka TRA uchukue tena Uba uende OSHA,uchukue tax uende NIDA sasa hivi mwekezaji akija pale TIC anapata huduma zote kwa hiyo ndio siri ya kuvutia wawekezaji wengi Tanzania” alisema Dkt Abbasi.







 Aliyasema hayo Novemba 6,2019 Ofisini kwake katika jengo la ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya miaka minne ya Rais wa awamu ya tano Dkt John Pombe Magufuli akiwa madarakani.

Rais Magufuli alichaguliwa na Watanzania Octoba 25, 2015 na kuapishwa November 5 mwaka huo huo wa 2015, na sasa anatimiza miaka minne huku Watanzania wakishuhudia akiimarisha maeneo mbalimbali yakiwepo ya uwekezaji.
Mwisho.

Post a Comment

0 Comments