Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

TIC yatoa Semina kwa Wabunge kuhusu uwekezaji.

Na Latiffah Kigoda- Dodoma.
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimepata fursa ya kutoa elimu ya uwekezaji  kwa Waheshimiwa/Wajumbe 
wa Kamati mbili za Bunge kupitia semina iliyoendeshwa 7Nov, Dodoma. 

Kamati hizo ni Kamati ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma na Kamati ya Katiba na Sheria. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania Profesa Longinus Rutasitara (wa kwanza kulia) 
 akita na Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw. Geoffrey Mwambe (wa pili) wakiandika 
baadhi ya maswali ya Wabunge ili wheeze kuyajibu kwa ufasaha 

Lengo la elimu hiyo ilikuwa ni kuwajengea Waheshimiwa Wabunge uelewa mpana wa masuala ya uwekezaji 
ambapo walipata fursa ya kufahamu kiundani majukumu ya TIC, namna Kituo kinavyovutia uwekezaji kwa kuzingatia 
Baadhi ya Wabunge walioshiriki katika Semina ya Uwekezaji iliyotolewa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania 
TIC iliyofanyika Jijini Dodoma Novemba 7,2019 wakisikiliza mada ya uwekezaji iliyowasilishwa na
Mkurugenzi wa Kituo hicho Bw. Geoffrey Mwambe

hitaji la mwekezaji, sababu za kuwekeza Tanzania, vigezo vya mwekezaji kujisajili na TIC, vivutio vya uwekezaji na 
namna ambavyo vinachangia kuvutia uwekezaji mpya, umuhimu wa uwepo wa dirisha la huduma za mahala pamoja 
TIC  kwa wawekezaji na namna linavyofanikisha uwekezaji, faida za uwekezaji, nafasi ya Tanzania katika masuala 
ya uwekezaji, mgawanyo wa miradi ya uwekezaji kimkoa, namna ambavyo miundombinu mizuri inavyochangia 
kuvutia uwekezaji, na namna ambavyo uharaka wa upatikanaji wa idhini(vibali,vyeti na leseni) mbalimbali za 
kufanikisha uwekezaji zinavyovutia uwekezaji. 

Vilevile Bw. Mwambe aliweka bayana  namna ambavyo mataifa yote duniani yanavyoshindana katika kuvutia 
uwekezaji, changamoto za uwekezaji na mapendekezo ya maboresho ya  mazingira ya uwekezaji nchini ili kuvutia 
uwekezaji zaidi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akiwasilisha mada katika 
semina wa Wabunge iliyofanyika Jijini Dodoma Novemba 7, 2019, Semina hiyo iliandaliwa na Kituo cha 
Uwekezaji Tanzania TIC.

Naye Mhe. Dkt. Chegeni (Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma) amezungumza kuwa, 
kupitia semina wameweza kupata picha kubwa ya mwenendo na nafasi ya Tanzania kiuwekezaji duniani, Afrika na 
Afrika Mashariki. 

Amesema, tayari kuna mikakati na jitihada zinazochukuliwa na Serikali kuboresha mazingira ya uwekezaji lakini 
tuongeze kasi ili kufanikisha uwekezaji zaidi. Semina imechangia kuwaobgezea elimu zaidi ya masuala ya uwekezaji 
na kwamba watakuwa katika nafasi nzuri ya kuchangia pale hoja za masuala ya uwekezaji zitakapowasilishwa 
Bungeni. Mhe. Chegeni amehimiza TIC iendelee kutoa elimu ya uwekezaji kwa wadau wote wakieleza TIC na 
majukumu yake, faida za uwekezaji kwa nchi na faida za mwekezaji akijisajili na TIC katika kufanikisha uwekezaji 
wake.



Post a Comment

0 Comments