Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Misri kuwekeza Tanzania kwenye Mbolea na Korosho


Dar Es Salaam.
Wawekezaji raia wa Misri wamewasili nchini kwa lengo la kuangalia fursa za uwekezaji kwenye sekta mbalimbali na wameonesha nia ya kuwekeza kwenye sekta ya  viwanda vya kubangua korosho na uzalishaji wa mbolea. 


Wawekezaji Raia wa Misri wakipata ufafanuzi kwa Maafisa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo Nchini Tanzania, Wawekezaji hao wameonesha nia ya kuwekeza kwenye zao la Korosho na Sekta ya Mbolea.

Hayo yamebainishwa na wfanyabiashara/wawekezaji wapatao kumi baada ya kutembelea Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kupokelewa na Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji Bw. John Mnali kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji.  

   Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Mathew Mnali (wa pili kutoka kushoto mwenye tai nyekundu) akizungumzia fursa za uwekezaji zilizopo nchini kwa Wawekezaji Raia wa Misri waliotembelea ofisi za TIC Desemba 11, 2019.

Katika majadiliano, wawekezaji hao wamepata fursa ya kupata taarifa na takwimu za hali ya uchumi, sababu za kuwekeza Tanzania,vivutio vya uwekezaji (vya kikodi na visivyo vya kikodi), usaidizi wa wawekezaji kupitia Mfumo wa Mahala Pamoja,jitihada zinazochukuliwa na serikali kuboresha miundo mbinu ya uwekezaji nchini na fursa zilizopo kwenye sekta/maeneo mbalimbali ikiwemo; kilimo na uongezaji thamani mazao ya kilimo, uchimbaji na uongezji thamani madini, uunganishwaji wa magari, utengenezaji wa madawa, ufugaji na uongezaji thamani mazao ya mifugo, uvuvi na uongezaji thamani mazao ya uvuvi, utalii, nishati na miundo mbinu.
 
Wawekezaji Raia wa Misri wakifuatilia Mada ya Uwekezaji iliyowasilishwa na Afisa Uhamasishaji uwekezaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bi. Diana Ladislaus Mwamanga, Mada ilihusu  fursa za uwekezaji zilizopo Nchini Tanzania, Wawekezaji hao wameonesha nia ya kuwekeza kwenye zao la Korosho na Sekta ya Mbolea.

Wageni hao wamefurahishwa na mapokezi waliyopata TIC na taarifa muhimu zenye ushawishi wa kuwafanya waamue kuwekeza nchini. Wageni hao watakuwepo kwa muda wa siku tatu ambapo pia watatumia nafasi hiyo kutembelea Taasisi/Mamlaka mbalimbali ili kujadili namna ambavyo watafanikisha uwekezaji wao sambamba na kutembelea Mkoa wa Mtwara ili kujionea fursa kwenye zao la korosho.

Post a Comment

0 Comments