Na Grace Semfuko, Dar Es Salaam.
Wahariri
wa vyombo vya habari nchini wameshauriwa kusimamia na kuandika habari za
kuvutia uwekezaji ili kuongeza kasi ya ujenzi wa viwanda ambavyo vitaajiri Watanzania wengi na kuongeza pato la Taifa litokanalo na kodi za Viwandani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw. Geoffrey Mwambe akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari wakati wa Semina ya kuwajengea uwezo wa kuandika Habari za Uwekezaji, Semina hiyo ilifanyika Ijumaa Desemba 6,2019.
Hatua
hiyo itasaidia kukuza sekta ya uwekezaji kwa kuanzisha miradi ya uwekezaji hatua
ambayo inatajwa kuwa kichocheo cha kuongeza pato na kukuza uchumi wa Taifa. Aidha,
uwekezaji huo pia utasaidia kuongeza ajira kwa wananchi na kuondokana na
utegemezi kwa baadhi ya vijana/wananchi ambao wengi ni nguvu kazi ya Taifa.
Hayo
yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw.
Geoffrey Mwambe wakati akifungua Semina ya siku moja ya Wahariri wa vyombo vya
habari nchini iliyokuwa na lengo la kuwapa elimu na kuwajengea uwezo na uelewa
mpana juu ya uwekezaji na namna ya
kuandika habari za kuvutia uwekezaji.
Baadhi ya Wahariri wa Vyombo vya Habari Nchini wakifuatilia kwa makini Mada ya Uwekezaji iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw.Geoffrey Mwambe, Semina hiyo ilifanyika Ijumaa Desemba 6,2019.
“Suala
la kutoa habari za kunadi fursa za uwekezaji nchini ni jukumu la TIC, hata
hivyo ili kulifanikisha inashirikiana na wadau mkiwepo Wahariri wa vyombo vya
habari na Waandishi wa habari,” alisema Mwambe
Akiendelea
na hotuba yake, Mwambe alisema suala la
uwekezaji Duniani ni la ushindani kwa kuwa nchi mbalimbali zikiwepo pia zilizoendelea
zinaangalia wawekezaji hao hao. Hivyo, kama timu tunatakiwa kufahamu kuwa
jukumu la kuvutia na kuhamasisha uwekezaji linatakiwa lifanywe kwa weledi wa
hali ya juu.
Wahariri
kama wadau wakubwa wa kuhamaisha na kuvutia uwekezaji nchini, kabla ya kuruhusu
habari yeyote ya masuala ya uwekezaji kwenda hewani, ni vema mkajiweka kwenye
nafasi ya Utanzania huku akiongeza kuwa wajibu wa Mtanzania yeyote bila kujali sehemu
aliyopo ni kuweka uzalendo na maslahi ya nchi mbele ikiwa ni pamoja na kuitangaza
ama kuinenea nchi mema.
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw.Geoffrey Mwambe akisisitiza jambo kwa Wahariri wa vyombo vya Habari kuhusu kuandika fursa za kuvutia Uwekezaji, Semina hiyo ilifanyika Ijumaa Desemba 6,2019.
Akiyataja
mema hayo Mwambe amesema kuwa ni pamoja na kunadi fursa za uwekezaji na
maliasili zilizopo Tanzania, kukaribisha wawekezaji, kueleza faida za
uwekezaji, na namna wawekezaji wanavyosaidiwa na Serikali kuanzisha miradi
nchini.
Mwambe
alihitimisha kwa kuwaomba Wahariri hao kupuuza kuandika habari za baadhi ya Taasisi,
Mamlaka ama mtu yeyote atakayejaribu kubeza jitihada zinazofanywa na Serikali
katika kuvutia na kuhamasisha wawekezaji kwa maslahi binafsi ama kwa lengo la
kuchafua nchi na kukatisha tamaa wawekezaji.
Naye
mwakilishi wa Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Elias Malima alisema nchi ipo katika
vita ya uchumi, na kuwataka Wahariri kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli zenye mlengo wa kuipaisha Tanzania kiuchumi na kuongeza kuwa Ofisi ya
Msemaji Mkuu wa Serikali haitasita kukichukulia hatua chombo cha Habari kitakachopotosha
masuala ya uwekezaji.
“Uwekezaji
ni suala la nchi Wahariri kama sehemu ya wadau tuna wajibu wa kuwa wazalendo
kwa kuisemea nchi na endapo atatokea mtu anachezea uwekezaji tupambae nae” alisema
Malima.
Miongoni
mwa mada zilizowasilishwa ni chanzo cha TIC, Mamlaka ya TIC, Urasimu
unavyokwamisha Uwekezaji na Wajibu wa Wanahabari kuandika na kutangaza fursa za
uwekezaji zilizopo Tanzania. Nyingine ni mchango wa tafiti mbalimbali kwenye
Uwekezaji na nafasi ya Tanzania kwenye Uwekezaji Duniani; Fursa, Vivutio na
Changamoto za Uwekezaji nchini Tanzania;
Huduma
zinazotolewa ndani ya Mfumo wa Mahala Pamoja katika kufanikisha Uwekezaji.
Sheria ya Uwekezaji na Huduma za kitaasisi kwa Wawekezaji; Mradi wa
e-regulation unavyosaidia wawekezaji na Jukumu la vyombo vya Habari katika
kuhamasisha na kuvutia uwekezaji.
0 Comments