Na Grace Semfuko, Songwe.
Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC
kimejipanga kuhakikisha wawekezaji wote wanajisajili kwenye kituo hicho ili
kupata fursa na taarifa mbalimbali za uwekezaji, kisheria na msaada wa huduma
za kikodi sambamba na kupata cheti.
“TIC ni chombo pekee cha kuratibu
uwekezaji hapa nchini hivyo tunayo kazi kubwa kuhakikisha elimu inawafikia
wawekezaji wa ndani, wan je na wananchi kwa ujumla kuhusiana na mazingira ya
uwekezaji na faida watakazozipata wanapojisajili TIC” alisema Bw. Ndwata.
Alisema katika Mkoa wa Songwe TIC itajikita zaidi kuwaelimisha wananchi pamoja na wawekezaji juu ya mazingira ya uwekezaji hapa nchini na umuhimu wa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za uwekezaji.
“TIC kushirikiana na Mkoa wa
Songwe pamoja na wadau wengine kutoka sekta binafsi tulihakikisha
tunawakutanisha wawekezaji wakubwa pamoja na wajasiriamali wadogo na wananchi
wa Songwe na mikoa ya karibu” alisema.
Ndwata alisema kuwa lengo ni kutangaza
vivutio vya uwekezaji na fursa zilizopo katika sekta mbalimbali za kiuchumi.
0 Comments