Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Serikali kuvutia mazingira ya uwekezaji

Na Grace Semfuko.
Serikali ya awamu ya tano tangu kuingia madarakani November 2015 imekuwa ikiboresha mazingira na kuvutia uwekezaji.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Agellah Kairuki alisema tangu kuingia madarakani kwa Rais Dkt John Pombe Magufuli hakuna kodi yoyote ya biashara na uwekezaji iliyoongezwa huku kodi zaidi ya 168 zikifutwa katika kipindi cha miaka miwili zikiwepo kodi 105 za kilimo.

Hatua hiyo inaonyesha ni kwa jinsi gani Serikali imedhamiria kukuza uchumi wa nchi kupitia biashara na uwekezaji.

Katika kuhakikisha uwekezaji unakua kwa kasi Serikali ya Tanzania pia inashirikiana na sekta binafsi kukuza sekta hiyo kwani wao ndio wenye mchango mkubwa kwenye uwekezaji wa sekta mbalimbali.

WAZIRI MKUU wa Jamhuri ya Tanzania Kassim Majaliwa mara kwa mara huwa anasema Serikali inaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia uwekezaji na biashara nchini.

ZAIDI YA SH. BILIONI 177 ZIMEPELEKWA HALMASHAURI-MAJALIWA-WAZIRI ...

Mhe. Kassim Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wizara yake ndio yenye jukumu kubwa la kusimamia uwekezaji, Waziri Mkuu anasema anasema mpaka sasa, hatua mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa kwa lengo la kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na biashara nchini. 

Majaliwa alifungua Kongamano la uwekezaji Juni 27, 2019 Jijini Dodoma na alisema ”Miongoni mwa hatua hizo ni uwepo wa usafiri wa uhakika na wa haraka wa abiria na mizigo kwa kujenga reli ya kiwango cha kimataifa (Standard GaugeRailway).” 

 

Mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR unaendelea, mradi huu ni mojawapo ya vivutio vya uwekezaji nchini Tanzania kwani utarahisisha usafirishaji.

kwa kuwa alikuwa Dodoma alitaja baadhi ya vivutio vitakavyorahisisha shughuli za uwekezaji  kuwa ni pamoja na usafirishaji ambapo uwanja wa ndege wa Dodoma umeboreshwa na kuruhusu ndege kubwa na ndogo kutua usiku na mchana.
  

”Mashirika ya ndege yanayotoa huduma yameongezeka na maandalizi ya awali ya ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa ndege katika eneo la Msalato yanaendelea.”

Waziri Mkuu amesema mkoa wa Dodoma una barabara za kuaminika za kiwango cha lami zinazoiunganisha na mikoa mingine pamoja na nchi jirani.


Amesema Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kuboresha huduma za afya na Dodoma kuna hospitali ya Benjamin Mkapa yenye uwezo kama wa Muhimbili na Mloganzila.
Amesema ujenzi wa mradi wa kufua umeme katika Mto Rufiji ‘Stiegler’s Gorge’wenye uwezo wa kuzalisha MW 2,115, utaongeza upatikanaji wa nishati ya uhakika nchini. 

“Mradi huo utaongeza upatikanaji wa umeme wa kutosha na wa uhakika kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya viwanda na uwekezaji nchini ikiwemo na katika mkoa wa Dodoma.

Mradi wa kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere (Stigler’s Gorge) uliopo katika bonde la Mto Rufiji ni miongoni mwa miradi mikuwa ambayo Serikali ya awamu ya tano unatekeleza, mradi huu utasaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika ambao utaimarisha uwekezaji wa viwanda nchini Tanzania.

Waziri Mkuu alisema Serikali itaendelea na utekelezaji wa mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (The Blue Print).
 

Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki alizungumza na Uwekezaji TV akasema nia ya Serikali ni kuendelea kuwa na mazingira wezeshi yanayowavutia wawekezaji nchini katika kuendelea kuchangamkia fursa zilizopo na kupokea maoni yao ili kutatua changamoto za kiuwekezaji.

“Serikali itaendelea kuweka mkazo mkubwa wa maboresho katika maeneo mbalimbali yatakayo kuvutia wawekezaji ikiwani pamoja na uboreshwaji wa sekta ya mawasilino, miundombiu ya barabara na usafirishaji ili kuwa na mazingira mazuri ya wawekezaji kuja kuwekeza nchini,”alisema Waziri Kairuki.

Aliongeza kuwa Serikali inaanza kutekeleza Mpango Kazi wa Uboreshaji wa Mazingira ya Biashara na Uwekezaji ambao tayari umefanyiwa maboresho na utekelezaji wake unatarajia kuanza mapema mwaka huu wa fedha wa 2020/ 2021.

Aidha waziri aliahidi kuendelea kusimamia maeneo muhimu ikiwemo ushiriki wa sekta binafsi katika maeneo ya uwekezaji na kueleza maboresho haya yatatekeleza hasa katika kuboresha mifumo na kuwa na maziringa mazuri yanayotabirika kwa wawekezaji.

“Kwa kutambua umuhimu wa Sekta binafsi, tutaendelea kusimamia ushiriki wao kikamilifu ili kuleta tija pasipo kubagua sekta hiyo na kuendelea kuwa na mifumo inayotabirika kwa ajili ya wawekezaji.



Makala imeandikwa na Grace Semfuko, Dar Es Salaam.

Post a Comment

0 Comments