Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

EWURA yatangaza kupungua kwa bei ya Mafuta, ni nafuu ya Uwekezaji.


Na Grace Semfuko
Bei za jumla na rejareja za mafuta ya petrol, dizeli na mafuta yalliyopokelewa nchini kupitia Bandari ya Dar es Salaam zimepungua ikilinganishwa natoleo lililopita la April 1 mwaka huu.

Taarifa kwa vyombo vya Habari iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Jijini Dar es Salaam jana na kusainiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mhandisi Godfrey Chibulunje ilieleza kuwa bei hizo zitaanza kutumika kuanzia leo Juni 6, 2020.
Kwa mujibu wa EWURA mabadiliko ya bei za mafuta katika soko la ndani yanatokana na mabadiliko ya bei za mafuta katika soko la Dunia na gharama za usafirishaji (BPS Premium).

Taarifa hiyo ilieleza kuwa Mwezi Mei,2020 bei za rejareja za petrol, dizeli na mafuta ya taa zimepungua kw ash.219 kwa lita (sawa na asilimia 10.50), sh. 143 kwa lita (sawa na asilimia 1.17) na sh. 355 kwa lita (sawa na asilimia 18.47 mtawalia).

Ikilinganishwa na toleo la mwezi uliopita bei za jumla za petrol, dizeli na mafuta ya taa zimepungua kwa sh 218.59 kwa lita (sawa na asilimia 7.63) na sh. 354 kwa lita (sawa na asilimia 19.69) mtawalia.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa bei za jumla za mafuta ya petrolina dizeli katika mkoa wa Tanga zimebadilika ikilinganishwa na toleo lililopita la April 1, 2020.

Kwa mwezi mei 2020 bei za rejareja za petrol na dizeli kwa mikoa ya kaskazini (Tanga,Arusha, Kilimanjaro na Manyara) zimepungua kw ash. 463 kwa lita (sawa na asilimia 21.88) na sh. 377 kwa lita (sawa na asilimia 18.21) mtawalia.
Kwa kulinganisha na toleo la mwezi uliopita wa April, bei za jumla za petroli na dizeli zimepungua kw ash. 461.82 kwa lita (sawa na asilimia 23.19) na shilingi 375.82 kwa lita (sawa na asilimia 19.33) mtawalia.

“Bei za mafuta ya taa kwa mikoa ya kaskazini zitaendelea kuwa zile zilizochapishwa katika toleo la April 1, 2020 kwa sababu hakuna shehena ya bidhaa hiyo iliyopokelewa nchini kupitia Babdari ya Tanga kwa mwezi April, 2020” ilieleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo mwezi mei 2020, bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya dizeli katika mikoa ya kusini (Mtwara, Lindi na Ruvuma) hazitabadilika ilikinganishwa na toleo lililopita la April 1, 2020 kutokana na kutokuwepo kwa shehena ya dizeli iliyopokelewa kupitia bandari ya Mtwara.

Hata hivyo bei za mafuta ya petrol zimepungua ikilinganishwa na toleo la mwezi uliopita.

Kwa mwezi Mei 2020 bei za jumla na rejareja za petrol zimepungua kwa sh. 129 kwa lita (sawa na asilimia 5.67) na sh 128.14 kwa lita (sawa na asilimia 5.99) mtawalia.

Kwa kuwa hakuna mafuta ya taa katika Babdari ya Mtwarawamiliki wa vituo vya mafuta ya taa wa mikoa hiyo wanashauriwa kununua mafuta hayo kutoka Dar Es Salaam na hivyo bei za rejareja za mafuta ya taa kwa mikoa hiyo zinatokana na gharama za mafuta hayo kutokea Dae es Salaam na kusafirishwa hadi mkoa husika.

EWURA imesisitiza kwamba bei kikomo za mafuta kwa eneo husika zinapatikana pia kupitia simu za mkononi kwa mujibu wa sharia ya mafuta ya mwaka 2015, bei za bidhaa za mafuta ya petrol zitaendelea kupangwa na soko na EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta.


Post a Comment

0 Comments