Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

KEDA yamkabidhi Ridhiwani Marumaru ya Mil.9

Kampuni ya KEDA inayotengeneza Marumaru kupitia kiwanda chake kilichopo katika Kitongoji cha Pingo, imemkabidhi box 200 za bidhaa hizo Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete.
Box hizo 200 zenye thamani ya shilingi milioni 9 zimetokana na ombi la Mbunge huyo alipofanya ziara jimboni humo ambapo alijionea miradi mbalimbali ikiwa kwenye hatua tofauti ambayo baadhi yake ina mahitaji ya vifaa hivyo.

Akizungumza baada ya zoezi hilo, Ridhiwani alisema hatua hiyo inakwenda kukamilisha miradi husika ambayo kwa asilimia kubwa inakaribia kumalizika.

“Kwa niaba ya Wakazi wa Jimbo la Chalinze naomba nitoe shukrani zangu za dhati kwa msaada huu ambao utaimarisha miradi yetu ya kijamii” alisema Ridhiwani Kiwete Mbunge wa Chalinze.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Kiwanda hicho Hussein Mramba alisema kwa kuona umuhimu wa kuimarisha miradi ya maendeleo ya kijamii katika Jimbo hilo wameamua kutoa Marumaru hizo ili kuweka mazingira mazuri kwenye miradi hiyo ambayo ni Kituo cha Afya na Shule mbalimbali.

Post a Comment

0 Comments