Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Mwekezaji wa Gesi Tanga ashauri masomo kwa vitendo


Mwekezaji wa Gesi aina ya Oxygen na Nitrogen mkoani Tanga Mohammed Noor ameishauri Serikali na Wamiliki wa Taasisi za Elimu nchini kuwapeleka wanafunzi wanaosoma masomo ya Sayansi kwenda kujifunza kwa vitendo kiwandani kwake ili waweze kujiongezea ufahamu wa vitendo katika masomo yao.

Aliyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kiwandani hapo ana kuongeza kuwa kiwanda chake ni kipya lakini ipo haja ya wanafunzo wa masomo ya sayansi kujifunza kwa vitendo.

“Upo umuhimu mkubwa wa Serikali pamoja na taasisi mbalimbali za Elimu nchini hususan Wanafunzi kuanzia shule za Sekondari na Vyuoni kuleta wanafunzi wao hapa ili wajifunze kwa vitendo, Mwanafunzi wa Sekondari Shuleni anajifunza kwa nadharia kuhusu matumizi ya gesi mbalimbali lakini hapa atakuja kujifunza kwa vitendo na atajionea namna inavyoandaliwa” alisema Bw. Noor.

Sambamba na hayo alisema endapo Wanafunzi wa masomo ya sayansi watakwenda kiwandani hapo kujionea matumizi ya kisayansi yanayofanyika katika eneo hilo watahamasika zaidi kulipenda somo hilo.

“ Wanafunzi wakijionea kwa matendo itasaidia sana kuongeza ari ya kujisomea na hatomaye kuongeza wataalamu katika sekta ya  gesi” alisema.

Post a Comment

0 Comments