Na Grace Semfuko.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Injinia Isack Kamwelwe amezindua safari za ndege za kusafirisha shehena ya minofu ya samaki kutoka Jijini Mwanza hadi Brassels Ubelgiji na Uholanzi kupitia Shirika la ndege la Rwanda ambapo mei 12 shirika hilo lilisafirisha tani nane za minofu hiyo ambayo itasafirishwa mara moja kwa wiki.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Injinia Isack Kamwelwe amezindua safari za ndege za kusafirisha shehena ya minofu ya samaki kutoka Jijini Mwanza hadi Brassels Ubelgiji na Uholanzi kupitia Shirika la ndege la Rwanda ambapo mei 12 shirika hilo lilisafirisha tani nane za minofu hiyo ambayo itasafirishwa mara moja kwa wiki.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe (wa pili kushoto) akikagua boksi la minofu ya samaki kabla ya kuingizwa kwenye ndege kwa ajili ya kusafirishwa moja kwa moja kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza kwenda Brussels nchini Ubelgiji.
Waziri Kamwelwe amewaagiza Wakuu
wa Mikoa ya Mwanza,Mara, Simiyu na Kagera kuunda mtandao wa pamoja wa wa
kuhakikisha Samaki wote wanaletwa kwenye kiwanda ili kurahisisha upatokanaji wa
minofu hiyo na kufikishwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwanza.
Kamwelwe amesema kwa sasa wameanza na zoezi la usafirishaji wa minofu ya samaki ambapo sasa wanajipanga kusafirisha bidhaa za nyama za ng'ombe na mbuzi ambapo amewataka wavuvi wadogo na wafugaji kuchangamkia fursa hiyo.
Kamwelwe amesema kwa sasa wameanza na zoezi la usafirishaji wa minofu ya samaki ambapo sasa wanajipanga kusafirisha bidhaa za nyama za ng'ombe na mbuzi ambapo amewataka wavuvi wadogo na wafugaji kuchangamkia fursa hiyo.
Katika hatua nyingine Serikali
imepokea injini mbili kutoka Nchini Korea Kusini ambazo zitafungwa kwenye Meli
mpya ya MV Mwanza.
Akizungumza Jijini Mwanza Waziri
Kamwelwe amesema Meli hiyo inayotengenezewa Jijini humo itakuwa ikifanya safari
zake kwenye Mikoa ya Mwanza-Bukoba na nchi
jirani za Kenya na Uganda.
Alisema Meli hiyo inagharimu
Shilingi Bilioni 159 na inatarajia kukamilika January 2021 na kuwataka
wakandarasi wa Gas Entec Co. Ltd, Kangnam Corporation zote kutoka Korea Kusini
zikishirikiana na Suma JKT ya Tanzania kuhakikisha zinakamilisha shughuli hiyo
kama mkataba unavyoelekeza.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe (wa pili kushoto) akikagua boksi la minofu ya samaki kabla ya kuingizwa kwenye ndege kwa ajili ya kusafirishwa moja kwa moja kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza kwenda Brussels nchini Ubelgiji.
Meli hiyo inayotajwa kuwa ni
kubwa kuliko zote katika Ukanda wa Maziwa Makuu, itakuwa na mita 92.6, Kimo chake
kitakuwa mita 11.2, upana mita 17 na uzito wa tani 3,500 kwa takwimu hizo ndio
itakuwa Meli kubwa kuliko zote na itakuwa inatumia masaa saba kutoka Mwanza
hadi Bukoba.
Akitoa ufafanuzi wa injini hizo
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli Tanzania (MSCL), Eric Hamisi amesema
injini hizo zimenunuliwa kwa Dola za Marekani 39,000,000 sawa na Shilingi
Bilioni 89.764 na kila moja ikiwa na tani 35 na uwezo wa kuzalisha KW 2,380.
Viongozi mbalimbali waliojitokeza kushuhudia usafirishaji wa minofu ya samaki yenye uzito wa tani nane kutoka uwanja wa ndege wa Mwanza moja kwa moja kwenda Brussels Ubelgiji wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Alisema uwezo huo wa injini
utaiwezesha meli hiyo kusafiri kwa saa saba kutoka Mwanza hadi Bukoba na kwamba
hadi sasa Wakandarasi wanaotengeneza wamelipwa Sh. Bilioni 55.618 sawa na
asilimia 64 ya gharama zote.
Mwisho.
0 Comments