Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Siku ya Nyuki Duniani na tija ya Uwekezaji.



Leo Mei 20, ni siku ya nyuki duniani.
Ni siku maalumu ya kutambua mchango wa nyuki duniani kote, katika mazingira, kilimo, ufugaji na uzalishaji wa asali.
Mbali na umuhimu wa asali kama chakula na dawa katika mwili wa binadamu, nyuki kamwe hawaishii kutengeneza tu asali.
Katika mchakato wa kutengeneza asali, nyuki hufanya kazi kubwa ya "Uchamvushaji" mashambani hivyo kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wingi mashambani.
Tanzania inaungana na mataifa mengine katika kuadhimisha siku hii ya nyuki Duniani huku ikikadiriwa kuwa kuna makundi milioni 9.2 ya nyuki wenye uwezo wa kuzalisha tani 138,000 za asali na tani 9,200 za nta kwa mwaka.

Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) ya mwaka 2017uwezo wa kuzalisha asali na nta kwa Tanzania unakadiriwa kuwa tani 138,000 na tani 9,200 mtawalia, hata hivyo uzalishaji ni tani 30,393za asali na tani 1,843 za nta kwa mwaka sawa na asilimia 22 kwa asali na asilimia 20 kwa nta kwa uwezo wan chi.aidha inaelezwa kuwa Tanzania inazalishatani 9,380 za asali na tani 625.3 za nta pekee kwa mwaka ambazo ni sawa na asilimia 7 tu ya rasilimali iliyopo.
Kutokana na upungufu huo wa uzalishaji na uhitaji mkubwa wa mazao ya nyuki, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS umekuwa ukifanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha watanzania wananufaika na fursa zilizopo kwenye sekta hiyo.
TFS inasaidia upatikanaji wa masoko ya mazao ya nyuki ndani na nje ya Tanzania, kutoa elimu na mafunzo mbalimbali ya ufugaji bora na wa kisasa wa nyuki, kutoa elimu kwa watanzania walaji kuhusu umuhimu wa asali pamoja na kuanzisha maduka ya asali.
Katika mahojiano na Gazeti la Mwananchi kuhusu maadhimisho ya siku ya nyuki Duniani mwaka huu wa 2020, Kamishna mhifadhi wa Misitu wa TFS Profesa Dos Santos Silayo alieleza namna ambavyo asali inachangia maendeleo ya nchi.
“TFS imeendelea kuimarisha shughuli za ufugaji wa nyuki jambo linalosaidia uzalishaji kuongezeka kuanzia mwaka 2015 hadi 2019, pia uzalishaji wa nta kwenye vituo vya uzalishaji vya wakala umeongezeka kutoka kilo 4,071 hadi kufikia kilo 30,000 sa asali na nta mtawalia” alisema Profesa Silayo.
Profesa Silayao anasema ili kuendeleza ongezeko la uzalishaji wa mazao ya nyuki na kama sehemu ya kuhamasisha uhifadhi na upandaji miti, Wakala umeandaa mkakati wa ufugaji wa nyuki kibiashara ambao unalenga kuongeza ufanisi katika shughuli za ufugaji nyuki katika vituo vyake.
Mkakati huo umewezesha wakala huo kuongeza uwekezaji wa shughuli za nyuki ili kuongeza uzalishaji
. Sekta ya ufugaji wa nyuki na uvunaji wa asali inahitaji uwekezaji kama ilivyo kwa sekta zingine hivyo wadau wadau mbalimbali wanahitajika kuweka nguvu zao katika uwekezaji huu ambao unaonyesha kuwa na tija ya kiuchumi kutokana na asali kuwa na soko kubwa la kimataifa.
Mbali na kuwa na soko kubwa la asali Duniani pia ufugaji wa nyuki unasaidia uhifadhi wa mazingira kutokana na mizinga ya nyuki kutengwa kwenye misitu ambayo husaidia kuwepo kwa hali nzuri ya hewa.
Faida nyingine ni kuongezeka kwa pato kiuchumi hususan kwa wananchi hasa waishio vijijini ambao ndio watunzaji wakuu wa mazingira, wakulina na wafugaji hawa wanaweza kuinua mapato kwa njia ya ufugaji nyuki.
Pia katika baadhi ya maeneo ufugaji wa nyuki unasaidia kupambana na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti hovyo, ujangili wa wanyama na uwindaji haramu ukataji miti kwa ajili ya mbao na uchomaji makaa. 
Kumekuwa na makampuni mbalimbali binafsi ambayo yanajishughulisha na uzalishaji wa asali nchini, lakini pia bado kuna fursa nyingi za uwekezaji kwenye sekta ya asali ili kuongeza tija hasa kwa wakati huu ambao wananchi wengi wanatumia asali kama kiburudisho, kiungo na dawa.
Anaandika Grace Semfuko, Dar Es Salaam.

Post a Comment

0 Comments