Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Maajabu ya Ziwa Chala, linafaa kwa Uwekezaji wa Utalii.


Pengine umeshawahi kusikia jina Chala mahali popote pale, iwe jina la Mtu au kitu fulani, sasa leo naomba nikueleze tu kwamba CHALA ni jina la Ziwa moja la maajabu lililopo Wilayani Rombo Mkoa wa Kilimanjaro, ziwa hili lipo kati ya mpaka wa Kenya na Tanzania, yaani kila nchi ina sehemu ya ziwa hilo.

Na Grace Semfuko, Rombo.

Ziwa Chala lina fursa za Uwekezaji katika Sekta ya Utalii kutokana na wageni wengi kuwasili katika eneo hilo kujionea maajabu ya ziwa hilo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)Bw. Geoffrey Mwambe akiangalia maajabu ya ziwa hilo lenye mandhari nzuri ya kuvutia, Mwambe na ujumbe wake kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania alifanya ziara ya kuangalia fursa za uwekezaji kwenye ziwa hilo.

Ziwa hili  la Chala lipo kati ya Tanzania na Kenya jirani na mpaka wa Holili. Chala ni la mtu, inasemekana Mzee huyo  na Familia yake alijitenga na jamii nyingine  na kuweka makazi  katika  moja ya vilima vinavyozunguka wilaya ya Rombo.



Mzee Chala inasemekana  takribani  miaka laki mbili iliyopita alikaa hapo na wakati huo kulikuwa na kilima kilichokuwa na volcano


Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)Bw. Geoffrey Mwambe akipata maelezo ya maajabu ya Ziwa hilo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Rombo Bi.Agnes Hokororo.

Volcano hiyo inahisiwa ililipuka dhoruba yenye kishindo kikubwa na matokeo yake kilima kilizama chini hivyo kufanya kilima kugeuka shimo kubwa lenye kina cha takribani  mita 300!

Mzee Chala na mji wake, Watoto,wake zake, mifugo na kila kitu vyote inasemekana vilizama kwenye shimo(cretor) hilo ambalo baadaye mkondo wa maji wa chini  kwa chini kutoka mlima mkubwa (mrefu) Afrika yaani Kilimanjaro yalibainika kujaza shimo hilo na kuwa ziwa!

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)Bw. Geoffrey Mwambe (mwenye koti) na Mkuu wa Wilaya ya Rombo Bi. Agness Hokororo (mwenye kitenge) wakiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Wilaya ya Rombo na Maafisa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) katika Ziwa Chala. 

Mkondo huo wa chini kwa kwa chini ulijaza cretor hilo ambalo kwa sasa Ziwa Chala badala ya kilima Chala lenye takribani ukubwa wa mita 500 urefu, upana mita 200 na kina yaani kwenda chini mita 300 (viwanja vitatu vya mpira wa miguu!.


Ziwa Chala linavyoonekana kwa upande mmoja eneo la Rombo.

Ziwa hilo la ajabu ambalo halina  mto unaoleta  maji kwa juu, huonekana kuwa na kina  kirefu kwa maana ya ujazo wa maji wakati wa kiangazi tu,  wakati ambao ukianangalia theruji ya Mlima Kilimanjaro huonekana kupungua kwa kuyeyuka kwa joto, lakini ziwa Chala huonekana kupungua kina au kukauka  wakati wa masika yaani kipindi cha baridi ambapo Mlima Kilimanajaro hunekana kufunikwa na theruji, hivyo kuthibitisha ziwa Chala kukosa maji ya kulijaza!

Licha ya mambo mengine ya ajabu kuonekana katika ziwa hilo ambyo mengi ni hadithi za viumbe vya ajabu kwa imani za mashetani,chunusi na mizimu kuonekana na vifo vya mara kwa mara kwa watafiti na watu wanoogelea, pikiniki na shughuli za utalii katika ziwa hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)Bw. Geoffrey Mwambe na Mkuu wa Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro Bi Agness Hokororo wakielekea eneo linapoonekana Ziwa Chala.

Kuna simulizi mbalimbali za kiimani zikihusisha ziwa hilo ikiwepo ile ya kila mwezi wa kumi na mbili ya kila mwaka, nyakati za usiku huonekana boti lenye taa ambayo huwa  linaelea majini kutoka upande mmoja kwenda kwingine, lakini Asubuhi huwa haionekani tena.

Simulizi nyingine ni Watafiti kutoka Ulaya walipandikiza viumbe hai kwenye ziwa hilo wakiwemo samaki wa maji baridi na mamba ili waone kama wanaweza kuishi humo na kuzaliana kwani awali hakukuwa na viumbe hai, baada ya mwaka mmoja wazungu hao sita walirudi kuona matokeo na kwa bahati mbaya mamba walikuwa wakubwa walipindua mtumbwi wao na  watafitti wawili kati yao wakageuzwa kitoweo wa mamba hao!

Wazungu walikasirika wakaenda kuleta nyama zenye sumu na mamba wote walionekana kuelea wakiwa wamekufa! kwa sasa ziwa halina mamba tena ila kuna samaki na kuna wakati wanaoneka nyoka wakubwa kama chatu na sawaka. Wito unatolewa kwa wizara husika, kutumia njia zake kutangaza ziwa hilo kama kivutio cha utalii.


Post a Comment

0 Comments