Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Sekta ya Maziwa ni Muhimu-Mwambe katika Ziara yake Kanda ya Kaskazini


Uwekezaji katika sekta ya maziwa umekuwa na umuhimu mkubwa kutokana na bidhaa hiyo kuwa na tija ya kiuchumi pamoja na kuongeza afya za wanywaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Geoffrey Mwambe alifanya ziara katika Kiwanda cha Maziwa cha Galaxy kilichopo Unga Limited katika Manispaa ya Arusha, na kubainisha kuwa takwimu za mpaka kufikia mwaka 2017  inakadiriwa kuwa Tanzania ni nchi ya pili Barani Afrika kuwa na mifugo mingi ikitanguliwa na nchi ya Ethiopia.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey Mwambe (Mwenye koti jeusi) akiuliza maswali kuonyesha anahitaji kujua jambo kutoka kwa viongozi wa Kiwanda cha maziwa cha Galaxy kilichopo Unga Limited Jijini Arusha alipotembelea kiwanda hicho Juni 2,2020. (Picha na Grace Semfuko)  

Alisema kwa mwaka huo wa 2017 ingawa Tanzania ilishika nafasi ya pili Afrika kuwa na idadi hiyo kubwa ya mifugo, ilikuwa ni ya 132 kwa nafasi ya unywaji wa maziwa kwa mtu mmoja kwani kiwango kilikuwa ni kunywa lita 40.29 tu kwa mwaka.

Kidunia nchi inayoongoza kwa unywaji wa maziwa ni Finlad ikikadiriwa kuwa mtu mmoja anakunywa lita 409 kwa mwaka.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey Mwambe akipata ufafanuzi kuhusu mashine hizo zinavyofanya kazi katika Kiwanda cha Maziwa cha Galaxy kilichopo Unga Limited Jijini Arusha (Picha na Grace Semfuko)

Kwa mujibu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi za mwaka 2016-2017 uzalishaji wa maziwa ulikuwa lita Bilioni 2.1 na udadi hiyo iliongezeka na kufikia lita Bilioni 2.4 kwa mwaka 2017-2018.

Aidha katika kipindi cha Julai 2017- April 2018, usindikaji wa maziwa umeongezeka na kufikia milioni 52.6 kutoka lita milioni 42.1 kipindi cha Julai 2016- April 2017.

Takwimu za mpaka kufikia Mei 2020 inaonyesha kuwa licha ya uzalishaji na usindikaji wa maziwa kuongezeka nchini bado mwenendo wa unywaji wa maziwa kwa mwananchi mmoja mmoja siyo wa kuridhisha.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey Mwambe akipata ufafanuzi kuhusu mashine hizo zinavyofanya kazi katika Kiwanda cha Maziwa cha Galaxy kilichopo Unga Limited Jijini Arusha (Picha na Grace Semfuko)

Kwa wastani mtu mmoja anakunywa lita 47 za maziwa kwa mwaka ikiwa ni pungufu mara nne ya kiwango kinachopendekezwa na Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa mtu mmoja kunywa lita 200 kwa mwaka.
Hii ndiyo hali halisi kwa takwimu chache za hivi karibuni kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi
Kiwanda cha Maziwa cha Galaxy kimesajili uwekezaji wake katika kituo cha uwekezaji Tanzania TIC na kinafanya kazi ya uzalishaji wa maziwa ili kukidhi mahitaji ya wanywaji katika kuongeza afya na kujipatia kipato kwa wakulima na wafugaji.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey Mwambe akionyeshwa mojawapo ya bidhaa za Maziwa yanayotengenezwa katika Kiwanda cha Galaxy  kilichopo Unga Limited Jijini Arusha (Picha na Grace Semfuko)

Nae Meneja wa Kampuni hiyo Bw. Irfan Virjee amesema tangu kujiunga kwao na TIC wamepata manufaa makubwa katika uwekezaji wao.

Kiwanda hicho kinachotengeneza aina mbalimbali za maziwa yakiwepo ya ya Mtindi, Yoghurt na maziwa fresh yanayokaa muda mrefu bila kuwekwa kwenye jokofu  kilipata cheti cha uwekezaji mwezi January mwaka 2018 baada ya kukidhi vigezo na wamewekeza kwa mtaji wa Zaidi ya dola Milioni 2.8.


Post a Comment

0 Comments