Header Ads Widget

Ticker

6/recent/ticker-posts

Tumefuta Tozo 117 za Biashara na Uwekezaji-Magufuli Bungeni Juni 16,2020


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Juni 16, 2020 amefunga rasmi Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kueleza kuwa katikia kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake, Sekta ya Uwekezaji imekuwa. 
Na Grace Semfuko, Dar es Salaam.

Aidha amesema wastani wa ukusanyaji wa mapato umeongezeka kutoka shilingi Bilioni 850 mwaka 2014/15 hadi kufikia shilingi Trilioni 1.3 mwaka 2018/2019. 

Rais amesema mafanikio hayo ya uwekezaji nchini yamekuja kufuatia kuwepo kwa mpango wa kuboresha mfumo wa udhibiti wa biashara (Blue Print) ambapo sheria mbalimbali zimerekebishwa na kurahisisha ufanyaji wa biashara na uwekezaji nchini.

Amesema katika kipindi cha uongozi wake jumla ya tozo na kodi mbalimbali 173 zimefutwa zikiwepo tozo 114 zinazohusu kilimo, mifugo na uvuvi na tozo nyingine mbalimbali.

“Wakati nazindua bunge hili niliahidi kukuza uchumi, tumejitahidi kutekeleza ahadi hiyo kwa kukuza sekta kuu za uchumi za uwekezaji, kuhusu sekta ya Viwanda ni viwanda vipya 8477 ambapo vikubwa ni 201 vya kati 460 vidogo 3,406 na vidogo sana ni 4460 hii imengeza idadi ya viwanda nchini, viwanda hivi vimeifanya nchi yetu kuzalisha ajira 482,601” alisema Rais Magufuli.

Aidha katika kuimarisha uwekezaji wa viwanda Rais amesema katika kipindi chake hicho Serikali imefanikiwa kupunguza tatizo la kukatika katika kwa umeme na katika kipindi hicho Tanzania haikuwahi kuingia gizani.

“Kwa kuzima mitambo ya kuzalisha umeme wa mafuta wa symbion, kwa kuzima mitambo ya IPTL, Aggreko na Symbion tumeokoa Shilingi Bilioni 719 kwa mwaka na hii ndio imewezesha TANESCO sasa ianze kujiendesha yenyewe” alisema Rais Magufuli.

Kuhusu sekta ya mawasiliano Rais Magufuli alisema Serikali imeboresha usikivu wa simu kutoka asilimia 79 ya mwaka 2015 hadi asilimia 94 mwaka 2019, pia idadi ya watumiaji wa simu na data imeongezeka, hii imechangiwa na kupungua kwa gharama za kupiga simu kwa dakika kutoka shilingi 267 kwa mwaka 2014/15 hadi shilingi 40 kwa sasa hivi alisema Rais Magufuli.

Katika Sekta ya afya Rais Magufuli alisema Serikali yake imefanikiwa kuongeza vituo cya kutolea huduma za afya ambapo Hospitali za Wilaya zimeongezeka na kufikia 71 na hospitali 10 za mikoa huku hospitali za rufaa za kanda zikiwa ni tatu ambapo watumishi ni zaidi ya watumishi 1,000 wameajiriwa kupitia ongezeko la hospitaloi hiyo.

“Tumefanikiwa kusomesha madaktari bingwa 301 ambao wameongeza huduma za wagonjwa wa moyo, figo na sikio, vifo vya watoto wachanga chini ya siku 28 vimepungua kutoka vifo 8 kwa mwaka 2015 hadi kufikia 7 kwa vizazi 1,000, na wagonjwa kutoka nje ya nchi sasa wameanza kuja kutibiwa Tanzania hususan wagonjwa wa moyo” alisema Rais Magufuli.

Post a Comment

0 Comments