‘Hongera
sana Wanawake wa TIC, nyie ni chachu ya mafanikio ya Kituo. Mjiamini,
mjiendeleze na muwajibike ipasavyo ili kuleta tija kwa
taasisi yetu na Taifa kwa ujumla’ Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Mwambe
Wanawake wa TIC katika maandalizi ya kuelekea ukumbi wa Mlimani City kusheherekea siku ya Wanawake Duniani |
Leo
tarehe 8 Machi, 2019, Kituo cha Uwekezaji
Tanzania (TIC) kimeungana na Wanawake wote nchini kusheherekea siku ya Wanawake
Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi. Sherehe hizo ambazo
zimefanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar es Salaam zimeshirikisha
Wanawake kutoka pande mbalimbali za nchi. Mgeni rasmi alikuwa ni Mhe. Paul
Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kauli mbiu ya mwaka huu ilikua ‘Badili
Fikra Kufikia Usawa wa Kijinsia kwa Maendeleo Endelevu’.
Wanawake wa TIC katika ubora wao |
Katika
kufanikisha tukio hilo muhimu, sherehe zilipambwa kwa maandamano, maonesho na utoaji
wa elimu kwa Wanawake kupitia hotuba ya Mgeni Rasmi na Viongozi mbalimbali
walioshiriki pamoja na mada zilizowasilishwa kuhusu mifuko ya uwezeshaji,
utaratibu wa kupata mikopo Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu na fursa
mbalimbali za kiuchumi.
Sehemu ya Wanawake wa TIC |
Kupitia
maadhimisho ya sherehe hizo ni wazi kwamba Wanawake wamebaini fursa mbalimbali za uchumi na TIC kama mdau wa masuala ya
uwekezaji inawahamasisha Wanawake wote kuchangamkia
fursa za uwezeshaji zinazotolewa na
taasisi za Serikali na sekta binafsi ili kuwekeza katika fursa mbalimbali za
uchumi nchini kwa maendeleo binafsi na Taifa kwa ujumla.
Wanawake wa TIC wakiwa katika ukumbi wa Mlimani City kusheherekea siku yao |
Kipekee
kabisa Mkurugenzi Mtendaji, Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Geoffrey Mwambe
katika siku hii muhimu ametoa hamasa kwa watumishi Wanawake wa TIC ambapo
amewakumbusha kutambua kuwa wao ni mhimili wa Kituo katika kutekeleza majukumu
yake hususan kuwahudumia wawekezaji katika kufikia malengo ya Serikali ya Awamu
ya Tano chini ya Mhe. Rais Dkt. John Magufuli yanayolenga kuwa na uchumi wa
kati kupitia viwanda ifikapo 2025.
TIC katika ukumbi wa Mlimani City
Picha tano kutoka chini zinawaonyesha Wanawake wa TIC katika pozi mbalimbali ikiwa ni kusheherekea siku ya Wanawake Duniani.
|
0 Comments