Wilaya hiyo tayari imejenga
kadhaa vikubwa kikiwepo cha Viazilishe na kiwanda cha Chaki.
Profesa Riziki Silas Shemdoe-Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara
Hayo yalibainika katika
ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Profesa Riziki Shemdoe
baada ya kutembelea Kiwanda cha Viazilishe, Kiwanda cha kutengeneza Chaki
pamoja na Kiwanda cha Vifungashio Wilayani humo.
“Viwanda hivi
vitawanufaisha wananchi wa Wilayah ii kwa kutoa ajira na kuongeza thamani
baadhi ya mazao yanayolimwa hapa, nawaombeni wananchi mzalishe kwa wingi viazi
lishe kwa maana sasa soko lipo la uhakika” alisema Prof Shemdoe.
“Mmeonesha ni kwa kiasi
gani mnazingatia, mmetimiza agizo la Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Magufuli
la Tanzania ya Viwanda, ujenzi wa viwanda hivi ni chachu ya kufikia maendeleo
ya uchumi wa viwanda” alisema Profesa Shemdoe.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Dkt Fredric Sagamiko alisema ujenzi
wa kiwanda cha viazi lishe pekee ambachi kina uwezo wa kukausha tani moja na
nusu kwa siku umegharimu zaidi ya shilingi milioni 461.
Aliitaja changamoto ya
uhaba wa vikaushio (Solar Dryier) pamoja na mtaji wa kuendeshea kiwanda hicho.
0 Comments